Posts

Showing posts from March, 2023

Kaimu Mkurugenzi wa TPHPA Prof Joseph Ndunguru atuma ujumbe wa Wataalamu wa TPHPA na AVRDC

Image
Pichani: Kulia  Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru akisalimiana na  Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika ya World Vegetable Centre Ndg. Gabriel Rugalema Na Innocent Natai Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru amewataka wataalamu wa mamlaka hiyo kushiriki kikamilifu katika utekelezaji ya makubaliano ya mashirikiano na kituo cha  Africa World Vegetable Center  (AVRDC) ili kuhakikisha nasaba za mimea zinakusanywa na kuhifadhiwa kwa wingi. Prof. Ndunguru ameyasema hayo leo March 7,2023 baada ya kufanya ziara ya kutembelea ofisi za kituo hicho kinachojihusisha na utafiti,ukusanyaji na uboreshaji wa nasaba za mbegu za mboga mboga  kilichopo Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha. Aidha alisema kuwa katika mazungumzo waliyofanya wameweka makubaliano ya kushirikiana katika maeneo matatu na miongoni mwa makubaliano hayo ikiwa ni pamoja na kukusanya zaidi nasaba ka...

MATUMIZI YASIYOFAA NA UUZAJI WA VIUATILIFU BANDIA NI KIKWAZO KATIKA KUKABILIANA NA WADUDU WAHARIBIFU WA MIMIEA- TPHPA

Image
  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru Tanzania ,akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 1,2023 jijini Dodoma katika ukumbi wa Idara ya Habari, wakati akielezea majukumu na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru, akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 1,2023 jijini Dodoma, wakati akielezea majukumu na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo. Na Innocent Natai Matumizi yasiyosahihi ya viuatilifu na udaganyifu wa baadhii ya wauzaji wa viuatilifu na mazao ya mimea imekuwa kikwazo katika kukabiliana na wadudu waharibifu wa mimea nchini. Hayo yameelezwa jijini Dodoma leo Machi 1,2023 na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru wakati akielezea majukumu na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo. Prof.Ndunguru ame...