Posts

TPHPA Yaandaa Kizazi Kipya cha Wataalamu wa Kilimo Salama Kupitia Mafunzo kwa Vitendo

Image
 Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) inaendelea kuwa daraja muhimu la maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali nchini kupitia programu yake ya mafunzo kwa vitendo. Kupitia programu hii, wanafunzi hupata nafasi ya kujifunza kwa vitendo masuala ya udhibiti wa visumbufu vya mimea, usimamizi wa viuatilifu, afya ya mimea, karantini na taratibu za usafirishaji wa mazao, hivyo kuongeza uelewa wao wa nadharia na vitendo. Katika vituo vya TPHPA vilivyopo Makao Makuu Ngaramtoni, maabara ya Kibaha, pamoja na ofisi za kanda, wanafunzi hushirikiana bega kwa bega na wataalamu wa mamlaka hiyo katika shughuli za tafiti, ukaguzi wa viuatilifu, na utoaji wa elimu kwa wakulima. Pia hujifunza mbinu za uchambuzi wa viuatilifu na matumizi ya teknolojia za kisasa katika maabara, ikiwemo uchunguzi wa mabaki ya viuatilifu kwenye mazao na mazingira, jambo linalowawezesha kupata ujuzi wa kiufundi na wa kitaalamu. Kupitia mpango huu, TPHPA inalenga kuandaa kizazi kipya cha...

Ushirikiano wa TPHPA na WorldVeg Wazaa Matunda: Mashine ya Kukaushia Mbegu Yazinduliwa Arusha

Image
Kupitia ushirikiano mzuri uliopo baina ya Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) na World Vegetable Center – Tanzania, umefanikisha ununuzi wa mashine ya kisasa ya kukaushia mbegu. ambapo Agosti 14, 2025, Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Prof. Joseph Ndunguru, akiwa sambamba na Bi. Coleta Ndunguru, Mkurugenzi Mkazi wa World Vegetable Center – Tanzania, wameizindua rasmi mashine hiyo katika Kituo cha Taifa cha Hifadhi Nasaba za Mimea (National Plant Genetic Resources Centre – NPGRC) kilicho chini ya TPHPA, Uzinduzi huu unalenga kuimarisha uwezo wa kituo hicho katika kuhifadhi na kulinda mbegu muhimu za kilimo nchini. Prof. Ndunguru ameeleza kuwa mashine hii itasaidia kupunguza unyevu kwenye mbegu kwa kiwango kinachofaa, jambo litakaloongeza muda wa kuhifadhi na kuhakikisha ubora wake udumu kwa muda mrefu. Amesisitiza kuwa hatua hii ni sehemu ya jitihada za TPHPA katika kuboresha teknolojia na miundombinu ya kulinda rasilimali za kilimo, sambamba na kukuza usalama wa chakula n...

TPHPA Yaelimisha darasa la Wakulima walioratibiwa na SAGCOT Juu ya Mbinu Bora za Upigaji Sumu kwenye Mimea viwanja vya Nane Nane – Morogoro

Image
 USHIRIKIANO TPHPA NA SAGCOT WAIMARIKA ZAIDI,WAFANYA USHIRIKIANO KUFUNDISHA WAKULIMA  Wakulima kutoka maeneo mbalimbali ya Morogoro wamepata fursa ya kunufaika na mafunzo muhimu yaliyotolewa na Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) katika banda darasa la SAGCOT lililopo katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea  Viwanja vya Mwl.Julius Nyerere Morogoro. Kupitia Mtaalamu wake aliebobea Ndg. Samweli Mmari Mkaguzi wa Viuatilifu, TPHPA imetoa elimu ya kina juu ya mbinu bora za upigaji wa viuatilifu katika mimea, ikiwa ni sehemu ya juhudi za mamlaka hiyo kuhakikisha wakulima wanatumia viuatilifu kwa usahihi, salama na kwa tija katika kukabiliana na visumbufu vya mazao. Katika mafunzo hayo, wakulima walifundishwa namna bora ya:Kutambua aina sahihi ya viuatilifu kulingana na aina ya visumbufu,Kupima na kuchanganya viuatilifu kwa uwiano unaofaa,Kutumia vifaa vya kisasa vya kupulizia viuatilifu kwa ufanisi zaidi,Kujikinga kiafya wakati wa kupulizia (Personal Prot...

TPHPA Yaandika Historia: NPPO ya Kwanza Duniani Kutumia Teknolojia ya Portable DNA Sequencer Kutatua Changamoto za Kilimo

Image
Agosti 6, 2025 — Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph Ndunguru, ameongoza hafla ya uzinduzi wa matumizi ya teknolojia mpya ya Portable DNA Sequencer katika banda la TPHPA, kwenye Maonesho ya Nanenane yanayoendelea Viwanja vya Nzuguni, Dodoma. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Prof. Ndunguru amesema kuwa TPHPA kupitia Mradi wa Kuimarisha Huduma za Afya ya Mimea na Usalama wa Chakula (STREPHIT) imenunua vifaa 20 vya Portable DNA Sequencer. Vifaa hivyo vitatumika katika maabara na moja kwa moja mashambani kwa ajili ya uchunguzi wa haraka wa vinasaba vya viumbe mbalimbali. Amefafanua kuwa teknolojia hiyo haitumiki tu kubaini visumbufu vya mimea, bali pia husaidia katika tafiti za udhibiti wa magonjwa ya mimea, ufuatiliaji wa usalama wa chakula, na usimamizi wa ubora wa mazao kabla ya kuingia sokoni au kusafirishwa. Prof. Ndunguru amesisitiza kuwa matumizi ya kifaa hiki ni mapinduzi makubwa kwa sekta ya kilimo, kwani yatawawezesha wata...

Prof. Joseph Ndunguru aitabiria makubwa TPHPA miaka 3 ijayo "It will be the best-performing MPPO in Africa."

Image
Tarehe 5 Agosti 2025, katika majaribio ya pili ya kifaa cha Portable DNA Sequencer yaliyofanyika katika banda la Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Viwanja vya Nzuguni – Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Prof. Joseph Ndunguru, amesema kuwa TPHPA inakwenda kuwa Best MPPO (National Plant Protection Organization) barani Afrika ndani ya kipindi cha miaka mitatu ijayo, kutokana na ubunifu, weledi na matumizi ya teknolojia katika kutekeleza majukumu yake. Prof. Ndunguru amesema kuwa teknolojia ya Portable DNA Sequencer itarahisisha kwa kiwango kikubwa uchunguzi wa visumbufu vya mimea na magonjwa, hivyo kuwezesha hatua za haraka na sahihi za udhibiti. Hii itasaidia kulinda mazao ya wakulima, kukuza usalama wa chakula na kuongeza ushindani wa mazao ya Tanzania katika soko la kimataifa. Aidha, alisema kuwa TPHPA inaendelea kuwekeza kwenye tafiti, vifaa, na mafunzo ya wataalam wake ili kuwa taasisi bora zaidi barani Afrika. Kupitia mafanikio haya, Prof. Ndunguru alisisi...

TPHPA Yajidhatiti Kudhibiti Kweleakwelea ili Kuboresha Kilimo na Kuwezesha Utekelezaji wa Agenda 10/30

Image
Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imeongeza jitihada katika kudhibiti uvamizi wa visumbufu hatarishi, ikiwemo kweleakwelea, ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa kuboresha kilimo na kutekeleza Agenda 10/30   mpango wa kitaifa unaolenga kuongeza tija na ustawi katika sekta ya kilimo hadi kufikia mwaka 2030. Kweleakwelea ni ndege vamizi anayeshambulia na kuharibu mazao kama mpunga, alizeti, na nafaka nyingine, hivyo kuhatarisha usalama wa chakula na kupunguza kipato cha wakulima. Ili kukabiliana na changamoto hiyo, TPHPA kupitia wataalamu wake wa Kanda ya Mashariki imeweka mikakati madhubuti ya ufuatiliaji, tathmini, na udhibiti wa kweleakwelea kabla haijasababisha madhara makubwa mashambani. Akizungumza katika banda la TPHPA kwenye Maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Mwl. Julius Nyerere  Morogoro, Dkt. Mahudu Sasamalo, Mkuu wa Kanda ya Mashariki, alieleza kuwa TPHPA imeendelea kudhibiti kwa mafanikio maeneo yaliyoathiriwa, ikiwemo If...

TPHPA Yashiriki Maonesho ya Nane Nane Katika Mikoa Saba, Yatoa Elimu ya Ubunifu kwa Wadau wa Kilimo

Image
Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu (TPHPA) inashiriki kikamilifu Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane kwa mwaka 2025 katika mikoa saba ya Tanzania, ambayo ni Dodoma, Morogoro, Lindi, Simiyu, Tabora, Mbeya na Arusha. Ushiriki wa TPHPA umejikita katika kutoa elimu ya afya ya mimea, matumizi sahihi ya viuatilifu, mbinu za kisasa za kudhibiti visumbufu vya mimea, pamoja na taratibu za usafirishaji wa mazao ndani na nje ya nchi. Miongoni mwa vivutio vilivyojizolea umaarufu mkubwa kwenye baadhi ya mabanda ya TPHPA ni bundi, ambaye ameoneshwa kwa lengo la elimu juu ya mchango wake katika udhibiti wa panya mashambani. Bundi, kama mnyama wala panya wa asili, ni sehemu ya mbinu rafiki kwa mazingira ya kupunguza idadi ya panya wanaoleta athari kubwa katika uzalishaji wa mazao. Wananchi wengi wameonesha kuvutiwa na suluhisho hili la asili, wakilitaja kuwa ni njia bora mbadala isiyotegemea kemikali. Katika mabanda yote saba, wataalamu wa TPHPA wamejipanga kutoa elimu ya moja kwa moja kwa wakulima...