Posts

Showing posts from November, 2023

Mashirika ya Umma yasiyoshiriki Mashindano ya SHIMMUTA kikaangoni,Naibu Waziri Mkuu Mhe. Biteko atoa Maagizo

Image
  Na Innocent Natai Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati,  Dk. Doto Biteko amemtaka Msajili wa Hazina kufikia Jumanne asubuhi awasilishe maelezo ya kwa nini mashirika mengi ya Umma hayajashiriki Michezo ya SHIMMUTA inayoendelea jijini Dodoma, huku ikitambulika kuwa, mashindano hayo yalianzishwa na Serikali huku mlezi wake akiwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ametoa maelekezo hayo jijini Dodoma wakati akifungua Mashindano ya SHIMMUTA yanayohusisha Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi ambapo awali, Mwenyekiti wa Kamati ya SHIMMUTA, Roselyne Massama alimweleza Naibu Waziri Mkuu kuwa wanakumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya muitikio mdogo wa Mashirika ya Umma kushiriki mashindano hayo jambo ambalo linazorotesha mashindano hayo. “‘Viongozi Serikali kama tumekubaliana kufanya jambo fulani basi tulifanye, na kama tunaona halifai  basi bora tuliache, kuliko tunakubaliana kufanya kitu  halafu hatukifanyi, haiwezekani  viongozi w...

MAFUNZO YA 59 YA PM2 YALIYOTOLEWA NA TPHPA JIJINI ARUSHA YAFUNGWA RASMI LEO,UPIMAJI WA UELEWA KWA WASHIRIKI WATOA MATOKEO MAZURI

Image
Na Mariam Makombe Hayo yamejiri leo 17 novemba katika ukumbi wa Mamlaka uliopo Makao Makuu Ngaramtoni Arusha ambapo Kaimu Mkurugenzi Dr.Osmundi Ndomba ameyafunga mafunzo hafla iliyoshuhudiwa pia  na wajumbe wa Menejimenti. Akiongea katika hafla hiyo Mratibu wa mafunzo ndg.Jumanne amesema mafunzo hayo yamekuwa na matokeo mazuri sana ambapo upimaji wa awali siku ya Kwanza na wa mwishoni umetofautiana na matokeo  ya mwisho yamekuwa mazuri ambapo washiriki wamejibu maswali Kwa ufasaha ikionyesha ni ushahidi walielewa wanachofundishwa, akileta maombi yake kama mratibu kwa Mamlaka katika hotuba yake amesema anaomba ufanyike utaratibu wa kuundwa umoja wa wauza pembejea kila mkoa kwani italeta mafanikio makubwa katika kudhibiti .Pia ameomba kuongezea Kwa idadi ya Wakaguzi katika maduka ya Viuatilifu ili kuleta tija zaidi. Aidha Mkuu wa Idara ya Usimamizi wa Viuatilifu Dr  Oshingi Shilla akiongea katika hafla hiyo amewataka washiriki hao kwenda kutangaza Mamlaka ,pamoja na hilo am...

WATUMISHI TPHPA WA JENGEWA UWEZO WA MATUMIZI YA MFUMO WA OFISI MTANDAO (E- OFFICE)

Image
  Na Innocent Natai    Leo Novemba 7. 2023 Wafanyakazi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania(TPHPA) wamejengewa uwezo juu ya matumizi ya mfumo wa TEHAMA (Mfumo wa Ofisi Mtandao E- Office),mafunzo hayo yameendeshwa katika Ofisi za Mamlaka zilizopo Arusha Ngaramtoni Wafanyakazi hao wameshukuru kwa mafunzo hayo ambapo wameipongeza serikali kwa kuanzisha mfumo huu unaoenda kuipunguzia Mamlaka gharama za uendeshaji kuanzia kudurufu makabrasha Dkt. Sospeter Kabululu ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA amesema kuwa, mfumo huu utakuwa na manufaa kwa sababu unaenda kupunguza gharama za kuandaa makrabasha, itaokoa muda, huku akiwataka Wafanyakazi hao kuutumia mfumo huu kwa kadri ya maelekezo yatakayotolewa. Akitaja faida za mfumo huo amesema kuwa Mfumo wa Ofisi Mtandao umetengenezwa ili kuwezesha na kurahisisha shughuli za utawala za kila siku ndani ya Serikali. Shughuli hizo zinahusu mzunguko wa mafaili na nyaraka ndani na miongoni mwa taasisi za umma. Maml...

MKURUGENZI WA TPHPA AFUNGUA MAFUNZO YA 59 YA MATUMIZI SAHIHI YA VIUATILIFU KWA WAFANYABIASHARA NA WAKULIMA, AZUNGUMZIA KUFUNGUKA MASOKO YA KIMATAIFA

Image
Na Mariam Makombe - TPHPA  Leo hii 6/11/2023 Mkurugenzi wa TPHPA Prof.Joseph Ndunguru amefungua mafunzo ya 59 ya matumizi sahihi ya Viuatilifu yanayotolewa na Mamlaka ya Afya ya mimea na Viuatilifu TPHPA kwa wafanyabiashara na wakulima yenye lengo la kutoa elimu ya Matumizi sahihi ya Viuatilifu ili kuepuka madhara kwa binadamu na mazingira yanayotokana na Matumizi yasiyo sahihi . Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo Prof.Ndunguru amesema moja ya jukumu kubwa ya TPHPA ni kudhibiti matumizi ,utengenezaji na usambazaji wa Viuatilifu,kwa hiyo kwa kutoa mafunzo hayo ni moja ya utekelezaji wa shughuli za Mamlaka zenye lengo la kutoa elimu itakayosaidia  kupunguza athari kwa jamii na mazingira  kutokana na  matumizi yasiyo sahihi ya Viuatilifu. Sambamba na hilo amesema kuwa matumizi sahihi ya Viuatilifu ni muhimu kwani pamoja na kupelekea mimea kuwa na Afya na kuepuka athari mbalimbali lakini pia inasaidia katika kufungua masoko ya nje Kwa bidhaa zetu na hata kuongeza ...