Posts

Showing posts from April, 2025

TPHPA YATUMIA KONGAMANO LA PEMBEJEO MKOANI MBEYA KUWAASA WAKULIMA JUU YA MATUMIZI SAHIHI NA SALAMA YA VIUATILIFU

Image
Akifungua Kongamano hilo litakalofanyika kwa siku mbili Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi amewapongeza taasisi ya CropLife Tanzania kwa kuandaa kongamano hilo mkoani hapo kwani litawasaidia wakulima wengi kwa kuwaongezea uwezo na kuzidi kuimarisha uzalishaji wa mazao bora ya biashara pamoja na chakula. Ikiwa kama mshiriki mkuu wa Kongamano hilo, Mamlaka ya Afya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imetumia uwanja wa Kongamano hilo kuwafundisha wakulima  matumizi  Sahihi na Salama ya Viautilifu, Utambuzi wa visumbufu mbalimbali pamoja na njia za kuwadhibiti. Mdhibiti Ubora wa Viuatilifu kutoka TPHPA Ndg.Ramadhani Kilewa amewaasa wakulima kuzingatia maelezo yanayoandikwa kwenye vibandiko vya viuatilifu ili kuepusha matumizi ya Viuatilifu bandia, Kukosea na kutumia kiuatilifu kisichoendana na zao au visumbufu husika na pia Kujikinga dhidi ya Madhara yatokanayo na kutotumia viuatilifu kwa Usahihi na Usalama kwani viuatilifu hivi ni Sumu. Uwepo wa TPHPA Kongamano hilo unasisit...

Taasisi mbalimbali za Kimataifa zazidi kumiminika TPHPA kufanya Mashirikiano

Image
  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph Ndunguru, amepokea ugeni wa Maafisa wa Serikali ya Nigeria kutoka Taasisi ya Nigeria Agricultural Quarantine Service (NAQS) katika Ofisi za Mamlaka Makao Makuu Arusha, Aprili 9, 2025. Ziara hii ni sehemu ya jitihada za kukuza ushirikiano wa kimataifa katika masuala ya afya ya mimea na udhibiti wa viuatilifu. Lengo kuu la ziara hii ni kujifunza kutoka kwa uzoefu wa TPHPA katika kudhibiti na kudumisha viwango vya ubora wa mazao, hususan katika masuala ya usalama wa chakula na biashara za mazao ya kilimo. Wakati wa ziara, pande zote mbili zilijadili mikakati bora ya udhibiti wa magonjwa ya mimea na usalama wa chakula, na kubadilishana mawazo kuhusu mbinu bora za kuongeza ufanisi katika sekta ya kilimo. Prof. Ndunguru alielezea furaha yake kupongeza hatua hii ya ushirikiano, akisema kuwa ni muhimu kwa nchi zote kushirikiana ili kuboresha udhibiti wa afya ya mimea na kuhakikisha mazao yanayoingia ...