Dkt. Oshingi Shilla Afunga Mafunzo ya Wakaguzi wa Afya ya Mimea na Viuatilifu, Awasisitiza Weledi, Uadilifu na Utoaji wa Haki

Leo Juni 18, 2025, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Dkt. Oshingi Shilla, amefunga rasmi mafunzo ya wakaguzi wa afya ya mimea na viuatilifu yaliyofanyika kwa muda wa siku 10 katika ukumbi wa Maji House, Morogoro. Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Dkt. Shilla amewasisitiza washiriki kuwa na weledi, uadilifu na kuhakikisha utoaji wa haki wakati wa kuwahudumia wananchi. Katika mafunzo hayo, washiriki walipatiwa elimu kuhusu mifumo ya kisheria, taratibu za ukaguzi, mnyororo wa ushahidi (chain of custody), mifumo ya kikodi kutoka TRA, pamoja na matumizi ya mfumo mpya wa e-Kilimo. Mratibu wa mafunzo hayo, Ndugu Mussa Chidinda, alieleza hayo mbele ya mgeni rasmi, akisisitiza kuwa lengo kuu ni kuwawezesha wakaguzi hao kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi. Mafunzo haya yamehusisha wakufunzi kutoka ndani na nje ya Mamlaka na yamewahusisha jumla ya washiriki 70 ambao ni watumishi wa TPHPA kutoka kanda zote saba za Mamlaka. Aidha, vion...