Dkt. Oshingi Shilla Afunga Mafunzo ya Wakaguzi wa Afya ya Mimea na Viuatilifu, Awasisitiza Weledi, Uadilifu na Utoaji wa Haki















Leo Juni 18, 2025, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Dkt. Oshingi Shilla, amefunga rasmi mafunzo ya wakaguzi wa afya ya mimea na viuatilifu yaliyofanyika kwa muda wa siku 10 katika ukumbi wa Maji House, Morogoro. Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Dkt. Shilla amewasisitiza washiriki kuwa na weledi, uadilifu na kuhakikisha utoaji wa haki wakati wa kuwahudumia wananchi.

Katika mafunzo hayo, washiriki walipatiwa elimu kuhusu mifumo ya kisheria, taratibu za ukaguzi, mnyororo wa ushahidi (chain of custody), mifumo ya kikodi kutoka TRA, pamoja na matumizi ya mfumo mpya wa e-Kilimo. Mratibu wa mafunzo hayo, Ndugu Mussa Chidinda, alieleza hayo mbele ya mgeni rasmi, akisisitiza kuwa lengo kuu ni kuwawezesha wakaguzi hao kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.


Mafunzo haya yamehusisha wakufunzi kutoka ndani na nje ya Mamlaka na yamewahusisha jumla ya washiriki 70 ambao ni watumishi wa TPHPA kutoka kanda zote saba za Mamlaka. Aidha, viongozi wa idara, vitengo na kanda mbalimbali pia walichangia kuwajengea uwezo washiriki kwa kutoa mada na miongozo mbalimbali ya kiutendaji.


Kwa pamoja, TPHPA inaamini kuwa mafunzo haya yatakuwa kichocheo cha utekelezaji bora wa majukumu ya wakaguzi katika kulinda afya ya mimea, usalama wa chakula na mazingira nchini.

Comments

Popular posts from this blog

Ni TPHPA tena! yatwaa tuzo Mshindi wa Kwanza

TPHPA WAKABIDHIWA MAABARA YA KISASA ILIYOGHARIMU BIL.3.8, KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO ATOA MAAGIZO

Kanda ya Kaskazini yatolewa kimasomaso na TPHPA Mashindano ya SHIMMUTA 2024//Yatwaa Mataji Matatu huku ikiweka rekodi Maalumu