"TPHPA tumejipanga kuhakikisha tunatimiza adhma ya Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ya Tanzania tuilishe dunia" Prof Joseph Ndunguru








Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano TPHPA

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania(TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru amesema kuwa Mamlka hiyo imejipanga kuhakikisha inaboresha mazingira ya utoaji wa huduma za afya ya mimea mipakani na kutimiza adhima ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ya Tanzania tuilishe dunia katika mazao yale ambayo ni ya chakula ili kurahisisha biashara za mazao ya kilimo

Prof. Joseph Ndunguru ameyasema hayo Katika siku ya pili ya ziara yake ya kutembelea vituo vya Mamlaka,ambapo leo Mei 4/2023 amefanya  ziara katika kituo cha ukaguzi cha TPHPA(Tarake) kilichopo baina ya Tarakea Wilayani Rombo, Mkoani Kilimanjaro na Nchi ya Kenya,Ziara hiyo pamoja na mambo mengine ililenga kukagua na kutatua changamoto za vituo vya Mamlaka hiyo,katika ziara hiyo aliambatana na Mkurugenzi wa huduma saidizi TPHPA Ndug.Ahmada Suleman

“Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, imedhamiria kuhakikisha inaongeza  mauzo ya nje ya chakula mwaka hadi mwaka na kama Mamlaka tunataka kutimiza adhima ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ya Tanzania tuilishe dunia katika mazao yale ambayo ni ya chakula na itawezekana kwa sisi Mamlka kuboresha huduma za afya ya mimea na Watumishi kujituma ” alisema Prof. Joseph Ndunguru akizungumza na watumishi wa Mamlaka hiyo Mpaka wa Tarakea

Comments

Popular posts from this blog

Ni TPHPA tena! yatwaa tuzo Mshindi wa Kwanza

Kanda ya Kaskazini yatolewa kimasomaso na TPHPA Mashindano ya SHIMMUTA 2024//Yatwaa Mataji Matatu huku ikiweka rekodi Maalumu

Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA Apokea Makombe 6 yaliyopatikana Katika Mashindano ya Mei Mosi na SHIMMUTA 2024