HAFLA YA MAKABIDHIANO VIFAA VYA UBORESHAJI AFYA YA MIMEA YAFANA, KAIMU MKURUGENZI ABAINISHA MANUFAA YATAKAYOPATIKANA,AMTAJA RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN










Mamlaka ya Afya ya mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA)imepokea msaada wa vifaa wenye thamani ya Bil.2.2 kutoka FAO 10/10/2023 ambapo Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Naibu Waziri wa Kilimo Mh.David Silinde.

Akizungumza katika hafla hiyo Kaimu Mkurugenzi wa TPHPA Prof.Joseph Ndunguru pamoja na kuishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Kuwa mistari wa mbele kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo Kwa lengo la kuongeza ajira,kutanua masoko na hata kuiongezea Bajeti Wizara ya kilimo

Pia  amebainisha mafanikio yatakayopatikana kutokana na vifaa hivyo ambapo amesema vifaa hivyo vitadaidia katika kuongeza maduhuli ya Serikali Kwa maana ya kuongeza mapato kutokana na ufanisi utakaoongezeka kutokana na vifaa hivyo kurahisisha utendaji wa kazi ambapo upande wa magari yatasaidia katika ufuatiliaji katika katika ukaguzi ,aidha vifaa vitasaidia katika kudhibiti na uhakika wa chakula na malighafi ya viwanda,mbali na Hilo vitasaidia kugundua visumbufu vipya na kuvidhibiti hivyo kupelekea Kupunguza upotevu wa mazao kabla na baada ya kuvunwa.

Mbali na hayo amesema itapelekea kufunguka kwa  masoko mapya ya kilimo kwani udhibiti wa visumbufu itapelekea ubora wa mazao yatakayokuwa na ubora utakaofanya mazao yetu kukubalika na masoko ya nje hivyo kupelekea kufunguka kwa masoko  ambapo ndio dhamira kubwa pia ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuona sekta ya Kilimo inakua na kuleta mafanikio Kwa wakulima wanapata masoko ya mazao yao   nje ya nchi na kuboreka kwa maisha yao kwa ujumla

Comments

Popular posts from this blog

Ni TPHPA tena! yatwaa tuzo Mshindi wa Kwanza

TPHPA WAKABIDHIWA MAABARA YA KISASA ILIYOGHARIMU BIL.3.8, KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO ATOA MAAGIZO

Kanda ya Kaskazini yatolewa kimasomaso na TPHPA Mashindano ya SHIMMUTA 2024//Yatwaa Mataji Matatu huku ikiweka rekodi Maalumu