Posts

Showing posts from January, 2024

TPHPA yapiga hatua utekelezaji wa Agizo la Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan

Image
 Leo Januari 25, 2023  Dkt. Osmund Ndomba Akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) ameshiriki zoezi la Wakuu wa Taasisi za Umma zilizopo Mkoani Arusha na Halmashauri za Mkoani hapo la Utiaji Sahihi wa Mkataba wa Mfumo mpya wa Usimamizi na Utendaji kazi katika utumishi wa Umma PEPMIS (Public Employee Performance Management Information Sysytem) na Mfumo wa Usimamizi wa Utendaji kazi katika ngazi ya Taasisi PIPMIS (Public Institutions Performance Management Information System) hii ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anayelenga kuimarisha mifumo ya uwajibikaji inayowezesha viongozi na watumishi wa umma kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi wakati na mahali popote. Akizungumza Wakati wa Akifungua Hafla hiyo Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Ndg. Missaile Musa amesema kuwa Mfumo wa Usimamizi na Utendaji kazi katika utumishi wa Umma PEPMIS (Public Employee Performance Management Information Sysytem) u...

Mafunzo ya Siku Tano (5) kwa Wakaguzi wa Viuatilifu yahitimishwa, Prof. Ndunguru azungumza na Wahitimu

Image
Leo Januari 12, 2024 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania Prof. Joseph Ndunguru ameshirikia katika hafla ya kufunga Mafunzo ya Wakaguzi 32 Wa viuatilifu yaliyoendeshwa Mkoani Kilimanjaro Kwa Siku Tano (5) kwa msaada kutoka Umoja wa Ulaya (European Union)kupitia mradi unaofadhiliwa na ACP MEAs3,Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Kwa kushirikiana na TPHPA   Yakiwa na Lengo la Kuwajengea uwezo wa Kukagua biashara za Viuatilifu ili kusaidia uzalishaji salama wa chakula na ulinzi wa afya ya binadamu na mazingira Prof. Ndunguru Akibainisha faida ya mafunzo hayo amesema kuwa wataalam hao wanajengewa uwezo ili waweze kufanya majukumu yao ya ukaguzi kwa weledi jambo ambalo litapelekea  kulinda afya ya binadamu,mimea na mazingira. Pamoja na hayo mafunzo  yatapelekea kuongeza tija katika uzalishaji kwani ukaguzi utakapofanyika kitaalam na kuzuia yale yote ambayo yangepelekea kuharibu uzalishaji matokeo yake ni kuongezeka tija ka...

WAKAGUZI WA VIUATILIFU NA WATUMISHI WA TPHPA WAONYWA KUTOJIHUSISHA NA BIASHARA YA KUUZA VIUATILIFU

Image
Hayo yamejiri katika mafunzo yanayotolewa na FAO Kwa udhamini wa Umoja wa Ulaya kwa kushirikiana na TPHPA yanayoendelea jijini Moshi kwa  Wakaguzi wa Viuatilifu kutoka Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu (TPHPA). Akizungumza Afisa Sheria Mwandamizi wa Kitengo cha Sheria - TPHPA bi.Elizabeth Swai amefafanua vifungu  mbalimbali vilivyopo chini ya Sheria ya Mimea Na.4 ya 2020. Akifafanua kifungu cha 12 na 38 (b) alisema, vinapiga marufuku Wakaguzi wa Viuatilifu na watumishi wa TPHPA kujihusisha na biashara ya viuatilifu,akiongelea adhabu iwapo mtumishi atabainika na kosa hilo amesema atashtakiwa mahakamani na kuhukumiwa kwenda jela au faini ama vyote kwa pamoja .Hivyo amewataka kuzingatia masharti hayo ili kuepuka kuingia matatani. Pamoja na vifungu hivyo vilevile  ameelezea kuhusu Viuatilifu na vinyunyizi vinavyoingizwa nchini ni lazima viwe  vimesajiliwa na  kupata vibali ,pia wafanya biashara wa viuatilifu lazima wawe wamepata mafunzo ya matumizi sahihi na sa...

MKURUGENZI MKUU TPHPA AFUNGUA MAFUNZO KWA WAKAGUZI WA VIUATILIFU,ABAINISHA MAFANIKIO YATAKAYOPATIKANA ,ATAJA MWAKA 2024 KUWA NA MAFANIKIO MAKUBWA KWA MAMLAKA

Image
Hayo yamebainishwa Leo wakati Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya mimea na viuatilifu(TPHPA) Prof.Joseph Ndunguru akifungua mafunzo ya siku 5 kwa wakaguzi wa viuatilifu    kutoka TPHPA katika ukumbi wa PANAMA Hotel jijini Moshi ambapo Mkurugenzi huyo amebainisha manufaa ya mafunzo hayo kwa nchi na kwa Mamlaka. Akiongea mara baada ya kufungua mafunzo amesema mafunzo kwa Wataalam wa TPHPA katika maeneo mbalimbali ni moja ya  jukumu kubwa la Mamlaka ili kuhakikisha lengo la mamlaka kuhakikisha afya ya mimea linafikiwa . Akibainisha faida ya mafunzo hayo amesema kuwa wataalam hao wanajengewa uwezo ili waweze kufanya majukumu yao ya ukaguzi kwa weledi jambo ambalo litapelekea  kulinda afya ya binadamu,mimea na mazingira. Pamoja na hayo mafunzo  yatapelekea kuongeza tija katika uzalishaji kwani ukaguzi utakapofanyika kitaalam na kuzuia yale yote ambayo yangepelekea kuharibu uzalishaji matokeo yake ni kuongezeka tija katika mazao ambayo itapelekea uboreshwaji wa maso...