Uongozi wa TPHPA na Wafanyakazi washiriki kuaga Miili ya Waliofariki katika Ajali iliyotokea Ngaramtoni Arusha
Na Innocent Natai
Februari 27,2023 Katika Uwanja wa michezo wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Arusha, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru ,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPHPA Prof. Andrew Temu na wafanyakazi wa Mamlaka wameshiriki katika kuaga miili ya watu kumi (10) kati ya ishirini na tano (25)waliofariki katika Ajali iliyotokea Jumamosi ya Februari 24, 2024 ikihusisha lori mali ya Kampuni ya KAY Construction ya Nairobi, Kenya na magari mengine madogo matatu, ilisababisha vifo vya watu 25 na kujeruhi wengine 21.
Comments
Post a Comment