TPHPA WAKABIDHIWA MAABARA YA KISASA ILIYOGHARIMU BIL.3.8, KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO ATOA MAAGIZO
Hayo yamejiri 13/8/2024 katika kituo cha kudhibiti visumbufu vya mimea kibiolojia ambapo kilichopo Kibaha Mkoa wa Pwani ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Mh. Gerald Mweli.
Akiongea wakati wa kukabidhi Maabara hiyo kwa TPHPA mara baada ya yeye kukabidhiwa kutoka kwa Msimamizi wa Mradi TANIPAC Bwana Clepin Josephat Mh. Mweli amewataka TPHPA kulinda na kulitunza jengo hilo lakini pia kutokana na malengo ya ujenzi wa Maabara hiyo matokeo yaonekane na hatimae kuongeza uchumi wa nchi kutokana na kukua kwa biashara ya mazao."Tunatarajia sasa Maabara hii ilikalete matokeo kulingana na malengo ,sisi kama wizara tumefanya sehemu yetu nanyi pia mfanye aidha msisite pale mtakapohitaji ushauri au msaada wowote tuko pamoja nanyi tutafanya kazi kama timu" alisema Mh. Mweli.
Nae Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa TPHPA Prof.Temu ameishukuru serikali kwa kuwezesha kupatikana kwa Maabara hiyo kupitia Mradi wa TANIPAC ambapo amesema Bodi itahakikisha Maabara hiyo inaleta tija na matokeo mazuri kama ilivyokusudiwa.
Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea Tanzania Prof.Joseph Ndunguru ameishukuru serikalii kwa kuwajengea Maabara hii ya kisasa kwani itasaidia katika kurahisisha uchunguzi wa usalama wa chakula,uchunguzi wa mgonjwa ya mimea pamoja
Comments
Post a Comment