MAFUNZO YA KUWA JENGEA UWEZO WA KUFANYA TATHMINI ZA VIUATILIFU; KAIMU MKURUGENZI MKUU TPHPA NDUGU OSHINGI SHILLA AWATAKA WASIMAMIZI WA VIUATILIFU KUZINGATIA MAFUNZO WATAKAYOPATA ILI KULETA UFANISI KATIKA KAZI ZAO
Hayo yamejiri wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya namna ya uhakiki wa vihatarishi katika viuatilifu yanayoendelea katika ukumbi wa Kibo Palace ambapo Mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi Mkuu ndugu Oshingi Shilla amefungua mafunzo hayo.
Akiongea mara baada ya kufungua Mafunzo hayo ya kujengewa uwezo kwa watumishi wanaohusika na usimamizi wa viuatilifu amesema ndg.Oshingi amesema lengo la afunzo haya ni kuendeea kuwajengea uwezo watumishi wanaohusika na usimamiaji wa viuatilifu nchinj ili kuwaongezea ujuzi katika usimamiaji na si hivyo tu bali pia kuwataka wafuate utaratibu unaotakiwa katika uhakiki wa ubora wa viuatilifu na kutoa tathmini sahihi juu ya athari za viuatilifu ili kujua ubora na kuwakinga watumiaji wa viuatilifu ambao ni wa kulima..
Akiongelea kuhusu uwezeshaji endelevu kwa wasimamizi hawo amesema Mamlaka imejipanga na siku zote imekuwa ikifanya hivyo kuhakikisha mafunzo haya ni endelevu kwani kumekuwa na mabadiliko ya teknoloiia hivyo mafunzo hayo ni endelevu ili kuendana na mabadiliko yanayotokea kutokana na kuingia kwa teknolojia .
Aidha amewashukuru Swedish Chemical Agency (KEMl )ambao pia ni Washirika wao ambao wanasaidia katika kuwezesha mafunzo haya ndani ya nchi na nje ya nchi ambapo huwezesha pia baadhi ya watumishi kwenda kujifunza zaidi nchini Sweden.
Mafunzo haya ni endelevu na pamoja na mafunzo haya kutakuwa na miradi ya pamoja kati ya TPHPA na KEMI ambayo imepata ufadhiri kutoka Swedish development Agency (Sida) ili kuendelea kuimarisha usimamizi wa Viuatilifu nchini kuwa wenye tija na kufikia malengo ya Muda mrefu ya Mamlaka ya TPHPA.
Comments
Post a Comment