Prof. Joseph Ndunguru afika Maonesho ya Saba Saba, Atuma ujumbe kwa Wadau
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru ametoa rai kwa wadau mbalimbali wa Kilimo nchini kutembelea katika katika maonesho ya 48 ya kibiashara ya kimataifa (Saba Saba) Dar es salaam hususani katika banda la TPHPA ili kuweza kupata Elimu na Huduma Mbalimbali
Ameyasema hayo leo Julai 10, 2024 wakati alipotembelea katika maonesho hayo katika viwanja vya Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es salaam ambapo ameeleza kuwa TPHPA imeendelea kutoa elimu na huduma kwa wadau nchini ili kuhakikisha wanafikia adha ya Serikali ya kumkomboa Mkulima
"Wadau tembeleeni katika banda letu hapa Tent la Katavi mtapata kufahamu masuala mengi kuhusiana taratibu mbalimbali za kufanya biashara za mazao na viuatilifu." amesema Prof. Ndunguru
Katika ziara hiyo, Prof.Ndunguru alipata pia nafasi ya kutembelea katika mabanda mengine ya Taasisi na bodi zilizopo chini ya Wizara ya Kilimo
Aidha Maonesho haya yalianza Juni 28,2024 na yanayotarajiwa kuhitimishwa Julai 13.2024 Huku yakiongozwa na kauli mbiu isemayo "Tanzania mahali sahihi pa Biashara na Uwekezaji"
Comments
Post a Comment