LICHA YA KUWA PANYA NI KITOWEO MAARUFU CHAKWALE, WAKULIMA WAELIMISHWA KUWADHIBITI KWA SUMU KUEPUKA MADHARA





TPHPA - Gairo

Maonesho ya Samia  Kilimo Biashara Expo 2024 msimu wa 3 Gairo yamewafikia wananchi wa kijiji cha Chakwale ambapo Wataalam wa TPHPA waliopo katika maonesho hayo wamewapa  mafunzo wananchi na Wakulima namna ya kutumia Viuatilifu na jinsi ya kutumia mitego ya kutegea panya mashambani na namna bora ya kuwadhibiti kwa Sumu  majumbani.

Aidha wametahadharishwa kutowatumia kama kitoweo Panya ambao watakuwa wameuliwa kwa sumu kwani watawaletea madhara ya kiafya.

Akizungumza  Mwenyekiti wa CCM GAIRO Mhe. Danistani Daudi Mwendi amewataka wananchi hao  kujitokeza kwa wingi kesho 12/10/2024 katika  kufunga maonesho haya  kijijini Rubeho.


Sambamba na ilo kawasisitiza wananchi wakajiandikishe katika daftari la wapiga kura na wanaotaka kugombea nafasi za uongozi wakachukue  fomu  ili kugombea nafasi mbalimbali kwani ni haki yao.

Comments

Popular posts from this blog

Ni TPHPA tena! yatwaa tuzo Mshindi wa Kwanza

Kanda ya Kaskazini yatolewa kimasomaso na TPHPA Mashindano ya SHIMMUTA 2024//Yatwaa Mataji Matatu huku ikiweka rekodi Maalumu

Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA Apokea Makombe 6 yaliyopatikana Katika Mashindano ya Mei Mosi na SHIMMUTA 2024