WASAFIRISHAJI WA MAZAO WAHIMIZWA KUTUMIA BANDARI YA TANGA,WAHAKIKISHIWA KUWEPO HUDUMA BORA ZA UKAGUZI KUTOKA TPHPA



Hayo yamesemwa na Kaimu Afisa  Mfawidhi wa Kituo cha TPHPA kilichopo Bandari ya Tanga Bi Monica Sylvester Kuziwa ambapo amewataka Wasafirishaji wa mazao  nchini kuwa wazalendo na kutumia Bandari ya Tanga kusafirisha mazao yao  na kupata huduma bora za ukaguzi wa mazao hayo inayotelewa na Ofisi ya Kituo cha TPHPA  kilichopo bandarini hapo zinazofanyika kwa ufanisi wa hali juu. 

Akiongelea kuhusu uboreshwaji uliofanywa na  Serikali ya awamu ya sita kwa kuboresha Miundo mbinu kwa kuongeza kina cha bahari ambapo sasa Meli kubwa zinaingia katika Bandari  hivyo kwa wale wananitumia Bandari ya Mombasa wasisite kupitisha hapa mazao yao, aidha  wataepuke changamoto mbalimbali za kiutaratibu ikiwepo kuhakikisha mazao yamekaguliwa katika kituo cha TPHPA na kupata nyaraka za uthibitisho. 

Akiongelea kuhusu changamoto mbalimbali zitokanazo na wateja wao amesema changamoto kubwa ni uelewa wa utaratibu za kufuata ili kusafirisha mazao lakini kwa  wamekuwa wakitoa elimu kwa wasafirishaji  ili kuwaelimisha jambo ambalo limekuwa likisaidia katika kupunguza changamoto hizo.

Comments

Popular posts from this blog

Ni TPHPA tena! yatwaa tuzo Mshindi wa Kwanza

TPHPA WAKABIDHIWA MAABARA YA KISASA ILIYOGHARIMU BIL.3.8, KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO ATOA MAAGIZO

Kanda ya Kaskazini yatolewa kimasomaso na TPHPA Mashindano ya SHIMMUTA 2024//Yatwaa Mataji Matatu huku ikiweka rekodi Maalumu