Mafuriko Hanang: TPHPA yaunga Mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan

Na Innocent Natai Leo Disemba 14,2023 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru ameongoza kundi la Viongozi na Watumishi wa Mamlaka hiyo kutembelea na Kutoa Msaada kwa Waathirika wa Maafa ya Mafuriko Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara yaliyotokea Usiku wa kuamkia Disemba 3,2023 na kusababisha uharibifu wa Mali,Vifo na Majeruhi Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo Prof. Ndunguru amesema kuwa Mamlaka hiyo imeguswa na tukio hilo hivyo imekuja kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha waathirika wa Mafuriko Mkoani hapo wanasaidiwa ili waweze kurudi katika hali zao za kawaida, aidha pia ametumia wasaa huo kutoa pole kwa familia zilizopoteza wapendwa wao katika tukio hilo huku akiwaombea waliopata majeraha kupona haraka na kurejea katika shughuli za kulijenga Taifa Kupitia msaada huo Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatil...