Posts

Showing posts from May, 2025

Washiriki Mafunzo ya 62 usimamizi sahihi wa Viuatilifu (pestcide Management) PM2 Watakiwa Kutotanguliza Maslahi Mbele bali wazingatie miiko na taratibu

Image
Mafunzo ya siku 14 ya Usimamizi wa Viuatilifu(Pesticide Management) ya 62(PM2) yamehitimishwa Leo 30/5/2023 katika ofisi za makao makuu ya TPHPA, Ngaramtoni – Arusha, huku washiriki wakikumbushwa kuwa waadilifu na kuhakikisha hawatangulizi maslahi yao  mbele katika biashara ya uuzaji wa viuatilifu.  Akizungumza kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa TPHPA Mgeni rasmi ndugu Kengese katika   kufunga mafunzo hayo  aliwasisitiza washiriki kuwa wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa matumizi ya viuatilifu yanafanyika kwa kuzingatia kanuni, maadili ili kulinda  afya ya binadamu na kuhakikisha usalama wa chakula pamoja na mazingira bila kuweka maslahi yao binafsi mbele.   “Ni muhimu kutambua kuwa taaluma mnayobeba inahusisha uhai wa watu na usalama wa chakula chetu. Msiruhusu maslahi binafsi ya kifedha au ya kibiashara kuwa kikwazo cha kuwajibika kwa uadilifu, mkatoe elimu kwa wakulima ambao ndio wateja wenu kwa usahihi,"alisisitiza ndugu Kengese Mafunzo haya yali...

WAZIRI BASHE AAGIZA UNUNUZI WA NDEGE TATU ZAIDI KWA AJILI YA UDHIBITI WA VISUMBUFU VYA MIMEA NA MAZAO

Image
Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe, ameitaka Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) kuanza mara moja mchakato wa kununua ndege nyingine tatu za kunyunyuzia viuatilifu ifikapo kabla ya Julai 1, 2025. Agizo hilo amelitoa leo Mei 30, 2025, wakati wa hafla ya mapokezi ya ndege mpya ya kilimo aina ya Thrush 510P2+ iliyofanyika katika Uwanja wa TAA jijini Dodoma. Mhe. Bashe amesema hatua hiyo inalenga kuongeza uwezo wa taifa kukabiliana na milipuko ya visumbufu vinavyoharibu mazao kama Quelea quelea, viwavijeshi vamizi, na nzige, ili kulinda usalama wa chakula na kuongeza tija kwa wakulima. Ndege hiyo mpya, yenye uwezo wa kubeba lita 1,930 za viuatilifu na kufanya kazi angani kwa zaidi ya saa 4, ni hatua ya mapinduzi katika kilimo cha kisasa. Prof. Joseph Ndunguru, Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, amesema ndege hiyo pia itatumika kwa uchunguzi wa kisayansi katika milipuko ya visumbufu nchini. Bodi ya Wakurugenzi kupitia Mwenyekiti wake, Prof. Andrew Temu, imesisitiza dhamira ya k...

TPHPA YAENDELEA NA ZOEZI LA KUONDOA MAGUGU VAMIZI ZIWA VICTORIA – MWANZA

Image
Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) kupitia Ofisi yake ya Kanda ya Ziwa chini ya Kaimu Meneja, Bi. Mary Dominick Leina, leo Mei 21, 2025, imeendelea na zoezi la kuondoa magugu vamizi aina ya gugu maji yaliyoenea katika maeneo mbalimbali ya Ziwa Victoria, jijini Mwanza. Zoezi hili lilianza rasmi mwezi Februari 2025 na limekuwa likitekelezwa na wataalamu wa Mamlaka kwa kushirikiana kwa karibu na wadau wengine, likiwa na lengo la kudhibiti kuenea kwa gugu hilo hatarishi pamoja na kuchukua sampuli kwa ajili ya kufanya utafiti wa kina kuhusu athari zake katika mfumo wa ikolojia ya ziwa hilo. Wataalamu wa TPHPA wamekuwa bega kwa bega na Kamati Maalum iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, wakishirikiana na wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). Hadi sasa, utekelezaji wa zoezi hilo unaendelea vizuri huku juhudi zikiendelea kuhakikisha kuwa gugu maji linaondolewa kwa ufanisi na mazingira ya Ziwa Vict...

TPHPA YATOA ELIMU KWA WATAALAM WA PPD PEMBA JUU YA MATUMIZI NA USIMAMIZI WA UTEGAJI WA SUMU YA PANYA MASHAMBANI

Image
Pemba – Wataalam kutoka Mamlaka ya Afya ya mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) wameendesha mafunzo kwa watumishi wa Divisheni ya Plant Protection (PPD) Pemba kuhusu matumizi sahihi na taratibu za usimamizi wa utegaji wa sumu ya panya mashambani. Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa pamoja kati ya TPHPA na Serikali ya Zanzibar kupitia Wizara ya Kilimo ili kukabiliana na baa la panya waliokuwa wakisababisha uharibifu katika mashamba ya mpunga yaliyopo maeneo mbalimbali ya Pemba. Akizungumza katika mafunzo hayo Bi Christina Tewele  Amewasisitiza umuhimu wa kuzingatia hatua zote za kiusalama kabla, wakati na baada ya matumizi ya sumu mashambani. Aidha, alifafanua juu ya aina ya sumu inayotumika, vipimo sahihi vya kuchanganya, muda wa kuweka chambo, na mbinu za kutathmini ufanisi wa zoezi la utegaji. Wakiongea Wataalamu wa PPD wameishukuru TPHPA kwa mafunzo hayo a kuahidi kuwa watatumia elimu hiyo kwa kuhakikisha wanawasimamia wakulima. na kutoa maelekezo ili kuzuia madha...

TPHPA YADHIBITI HATARI YA UHARIBIFU WA MPUNGA MASHAMBANI :

Image
Yatoa Elimu  utegaji Sumu ya Panya mashambani na kusimamia Uchanganyaji wa sumu na Chambo Zanzibar Katika kuhakikisha usalama wa binadamu, mifugo, na mazingira wakati wa kudhibiti panya mashambani, Wataalam kutoka  TPHPA wametoa  elimu ya tahadhari kwa wakulima wa Zanzibar  kabla ya kuweka sumu ya kuua panya kwenye mashamba yao. Zoezi hili limefanyika katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar likiwemo eneo la Bumbwisudi, Cheju na Kilombero. Wakulima walipokea mafunzo ya kina kuhusu matumizi salama ya sumu, hatua za kuchukua ili kujikinga na madhara, na umuhimu wa kushirikiana na wataalamu katika hatua zote za utegaji. Wataalam hao walisisitiza tahadhari muhimu kama kuhakikisha Sumu haitumiki ndani ya nyumba, kuwepo kwa alama ya kitambaa chekundu  katika Shamba lililotegwa  sumu ili kujulisha hatari katika eneo hilo, Watoto na mifugo wasikaribie eneo lenye sumu. Vilevile Vifaa vilivyotumika kubebea au kuchanganya sumu (mfano mifuko) vichomwe moto baada ya matumiz...

TPHPA YASHIRIKIANA NA PPD ZANZIBAR KUKABILI BAA LA PANYA MASHAMBANI,HEKA 700 ZA MAZAO ZADHIBITIWA KUTOKANA NA PANYA WAHARIBIFU

Image
Katika jitihada za kuimarisha usalama wa chakula na kulinda uzalishaji wa mazao visiwani,  TPHPA kwa kushirikiana na Divisheni ya Plant Protection ya Zanzibar kupitia Wizara ya Kilimo, wanafanya ushirikiano kwa pamoja ya kudhibiti baa la panya kwa kutumia sumu iliyotolewa na TPHPA.  Zoezi hili  ni kufuata ombi  kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa TPHPA, likiwa ni sehemu ya mpango wa haraka kukabiliana na baa la panya  waharibifu  katika  mashamba ya Mpunga yenye kubwa wa heka takriban 700 kwa Unguja na Pemba. Kupitia ushirikiano huo, TPHPA imepeleka wataalam wake visiwani kwa ajili ya kusimamia zoezi zima la maandalizi, utoaji wa elimu ya namna ya udhibiti kwa wakulima, pamoja na uchanganyaji na usambazaji wa sumu kwa uangalizi wa kitaalamu. “Huu ni mfano bora wa ushirikiano kati ya taasisi za Muungano. "Tumepokea sumu kutoka TPHPA baada ya kuwasilisha mahitaji yetu, na wamekuja pamoja na wataalamu wao ku...

SIKU YA KIMATAIFA YA AFYA YA MIMEA YAADHIMISHWA ARUSHA, DKT. NINDI ASISITIZA DHANA YA “AFYA MOJA”

Image
Arusha, 12 Mei 2025– Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Afya ya Mimea yamefanyika katika viwanja vya Makumbusho ya Azimio la Arusha, yakiwa ni ya pili tangu kuanzishwa kwake mwaka 2024. Kaulimbiu ya mwaka huu ilikuwa “Umuhimu wa Afya ya Mimea katika Afya Moja,” ikilenga kuelimisha umma kuhusu mchango wa afya ya mimea katika maisha ya binadamu, ustawi wa wanyama na mazingira. Akizungumza katika maadhimisho hayo kama mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Umwagiliaji na Ushirika, Dkt. Stephen Nindi, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia dhana ya “Afya Moja” inayounganisha sekta za afya ya binadamu, wanyama na mimea kwa lengo la kufanikisha ustawi wa pamoja. “Afya ya mimea ni msingi wa uzalishaji wa chakula na afya ya binadamu. Hatutakuwa salama endapo tutapuuza kipengele chochote cha mfumo wa ikolojia,” alisema Dkt. Nindi. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph Ndunguru, alieleza kuwa Tanzania kupitia TPHPA imef...