KAIMU MKURUGENZI TPHPA PROF.JOSEPH NDUNGURU AMPONGEZA RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUWEKA NGUVU KATIKA SEKTA YA KILIMO

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Afya ya mimea na Viuatilifu(TPHPA) Prof.Joseph Ndunguru ametoa pongezi hizo wakati akifungua Mkutano wa mwaka wa Tanzania Entomological Association (TEA) uliofanyika New Safari Hotel Arusha ambapo yeye alikuwa Mgeni rasmi. Akizungumza amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr.Samia Suluhu Hassan amejikita katika kuleta mabadiliko kwenye sekta ya Kilimo na kuhakikisha anaweka nguvu nyingi katika kuhakikisha kilimo kinakuwa na kukuza uchumi wa nchi yetu na si hivyo tu lengo lake ni kuona Tanzania inalisha dunia Jambo ambalo linawezekana wote Kwa pamoja tukiweka juhudi na kufanya kilimo cha kisasa. Aidha Kaimu Mkurugenzi huyo amewataka wanachama hao kukutana mara kwa mara ili kwa pamoja kujadili changamoto za wadudu waharibifu wanaoleta uharibifu katika mazao ya kilimo na kuja na utatuzi thabiti ili kumaliza tatizo hilo na kufanya kilimo kiwe chenye tija na kukuza uchumi. Akiongelea suala la kuwawezesha ...