Posts

Showing posts from March, 2024

WAJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI TPHPA WATEMBELEA OFISI ZA TPHPA NAMANGA,WAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU

Image
  Wajumbe wa bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Afya ya mimea na Viuatilifu  wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Prof.Andrew Temu 19 Machi 2024 wametembelea ofisi za Mamlaka  zilizopo mpakani mwa Kenya na Tanzania Namanga pamoja na Kituo cha kijasusi cha ukusanyaji wa taarifa za masoko nje ya nchi,lengo likiwa ni kujionea shughuli na changamoto mbalimbali kwa ajili ya kupata ufumbuzi. Akiongea mara baada ya ukaguzi sehemu mbalimbali za utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka kama vile eneo la ukaguzi,maabara Prof.Andrew Temu amewapongeza kwa namna wanavyofanya kazi kwa kushirikiana na taasisi zingine 18 za serikali zilizopo mpakani hapo lengo likiwa ni kufikia matakwa ya serikali,"Kwa ushirikiano huu niliouona hapa naahidi kuwa balozi wenu nitalisemea hili kila mahali nitakapokwenda aidha nawapongeza sana mamlaka kwa jinsi mnavyochapa kazi katika kuhakikisha sheria zinafuatwa na kuondoa ukiukwaji unaoweza kuleta madhara kwa afya zetu na uchumi wa Tanzania,mna wajibu mkubwa w...

TPHPA yawajengea uwezo wa Matumizi sahihi na Salama ya Viuatilifu wakulima wa Mazao ya Viungo na Mpunga Mkoani Morogoro

Image
Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) kupitia Kitengo cha Usimamizi wa Teknolojia na Vinyunyizi vya Viuatilifu (PAT) imeto mafunzo ya Matumizi Sahihi na Salama ya Viuatilifu kwa Wakulima wa Mazao ya Viungo na Mpunga katika Wilaya za Mvomero na Morogoro vijijini zote zikipatikana katika Mkoa wa Morogoro. Machi 18,2024 Akizungumza katika Mafunzo hayo Dkt. Magreth Mwangi amesema kuwa mafunzo hayo yamefanyika katika Kata Tano (5) katika Wilaya hizo ambapo mafunzo hayo yalilenga kuwezesha wakulima kulima kilimo salama na chenye tija kwa kupulizia Viuatilifu wakiwa wamejikinga na kuhifadhi maeneo salama vifungashio vya Viuatilifu vilivyotumika. Kwa upande wao Wakulima wa Kata hizo waliopata mafunzo hayo wamewashukuru wataalamu hao Kwani kabla ya Mafunzo hayo wameeleza kuwa walikuwa wakitumia Viuatilifu Vingi bila kufuata taratibu hivyo kupata hasara za mazao na kifedha,pia wamesema walikuwa wakiathirika na viuatilifu bila wao kujua kutokana na tabia ya kutokuhifadhi vi...