Posts

Showing posts from January, 2023

HABARI PICHA:DKT. OSHINGI SHILLA AFUNGUA KIKAO MAALUMU CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA TPHPA

Image
  Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Usajili na Udhibiti wa Viuatilifu  Dkt Oshingi Shilla , akisisitiza jambo wakati akifungua  Kikao Maalum cha Baraza la wafanyakazi la Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) kilichofanyika January 20, 2023 katika ukumbi wa Mikutano wa  Mamlaka Hiyo Jijini Arusha . Agenda ya kikao ikiwa ni kujadili bajeti ya Mwaka 2023/2024 ambapo Miongoni mwa vipaumbele vya bajeti ya hiyo ikilenga kulipa mapunjo ya mishahara na madeni ya wafanyakazi (Picha na Innocent Natai) Picha mbalimbali zikionesha wajumbe wa  Kikao Maalum cha Baraza la wafanyakazi la Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) kilichofanyika January 20, 2023 katika ukumbi wa Mikutano wa  Mamlaka Hiyo Jijini Arusha   wakichangia ajenda  

HABARI PICHA :WATUMISHI WA MAMLAKA WAENDELEA KUPATIWA ELIMU YA MATUMIZI YA MFUMO WA ULIPAJI SERIKALINI (MUSE)

Image
Na Innocent Natai  JANUARI 19/2023 Picha na Matukio mbalimbali zikionyesha  washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa Ulipaji Serikalini(MUSE) yanayoendelea  katika Ofisi za Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania zilizopo Arusha ,Kukamilika na kuanzwa kutumiwa kwa Mfumo huo kunatarajiwa kusaidia  kuongeza makusanyo ya mapato, utarahisisha ulipaji wa fedha pamoja na kutunza kumbukumbu za matumizi ya fedha. Aidha   Mafunzo hayo yamewahusisha Wahasibu, Meneja wa Fedha, Wataalam wa Manunuzi, Maafisa TEHAMA na Maafisa Bajeti,Mafunzo hayo ya natarajiwa kumalizika ndani ya wiki mbili yakilenga kuwajengea uwezo wa kuutumia vilivyo mfumo huo.

KAIMU MKUU WA SEHEMU YA USAJILI NA UDHIBITI WA VIUATILIFU AONGOZA KIKAO CHA KUANDAA BAJETI YA MAMLAKA YA 2023/24 JIJINI ARUSHA

Image
Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Usajili na Udhibiti wa Viuatilifu Dkt Oshingi Shilla , akisisitiza jambo wakati wa kikao cha kuandaa bajeti ya Mamlaka ya 2023/24. Kikao hicho kimefanyika Januari 18, 2023 jijini Arusha ikiwa ni maandalizi ya kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Mamlaka hiyo kitakachofanyika Januari 20, 2023. Sehemu ya Wajumbe wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania wakiwa kwenye kikao cha kuandaa Bajeti ya Mamlaka kwa Mwaka 2023/24. Kikao hicho kimefanyika Januari 18, 2023 jijini Arusha ikiwa ni maandalizi ya kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Wakala hiyo kitakachofanyika Januari 20, 2023. Na Innocent Natai Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Usajili na Udhibiti wa Viuatilifu Dkt Oshingi Shilla , Januari 18,2023 kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka amefungua kikao cha bajeti ya Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) ya mwaka 2023/24 kikao kilichojumuisha wakuu wa idara,vitengo na wakuu wa kanda kilichofanyika  katika ukumbi wa Mikutano wa Mamlaka...