Posts

Showing posts from February, 2024

WASHIRIKI PM2 IRINGA WAELEZWA UMUHIMU WA MAVAZI KINGA ILI KUEPUKA MADHARA

Image
Ikiwa ni siku ya tatu katika mafunzo yanayoendelea kwa Wakulima ,Maafisa kilimo ,wafanyabiashara wa viuatilifu mkoani Iringa Mkufunzi wa Mafunzo ndg.Jumanne amewatahadharisha uzingatiaji wa mavazi kinga wakati wa kutumia viuatilifu ili kuepuka madhara mbalimbali ya muda mrefu na mfupi yanayoweza kutokea iwapo mavazi kinga hayatazingatiwa. Akieleza wakati akifundisha mada hiyo ndg.Jumanne amesema wakulima hawana budi kuzingatia uvaazji wa mavazi yanayotakiwa muda wote wanapotumia viuatilifu ili kuepuka madhara yanayoweza kuwapata kupitia ngozi,pua au katika macho,akikazia hilo ndugu Jumanne amewakumbusha kuwa viuatilifu ni Sumu hivyo kila anaetumia hana budi kujikinga. Akitaja baadhi ya vifaa kinga hivyo vinavyokuwezesha kusaidia viuatilifu visiingie mwilini kupitia sehemu mbalimbali za mwili  amesema ni mabuti ya mpira,gloves za mpira,Miwani maalum,vichuja sumu,makoti marefu ya mpira ,kofia

Tumieni Mikutano ya Baraza la Wafanyakazi kuongeza ufanisi Kazini. -Prof. Andrew Tumu

Image
 Watumishi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) wametakiwa kutumia mikutano ya Baraza la wafanyakazi kujadili mambo yanayoleta tija kwa ajili ya kuimarisha utendaji wa kazi miongoni mwao ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea. Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPHPA  Prof. Andrew Temu alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi la Kwanza la Mamlaka hiyo mapema leo Februari 27,2023 katika mkutano uliofanyika ndani ya ukumbi wa mikutano wa Mamlaka hiyo Arusha Ngaramtoni. Akizungumza katika mkutano huo Prof.Temu amesema ili kufikia malengo ya Mamlaka hiyo ambayo ni pamoja na kuifanya Tanzania kuongeza Kufanya biashara ya mimea na mazao hapa nchini na kimataifa ni muhimu kufanya kazi kwa ufanisi na kutumia vyema Baraza la wafanyakazi kwa kuzungumzia Mipango ya kusaidia Mamlaka hiyo. Amefahamisha kuwa TPHPA ni taasisi ya kisayansi, RAAWU ni chama cha wafanyakazi kwenye tasisi za elimu ya juu, sayansi, tekinolojia na u...

Uongozi wa TPHPA na Wafanyakazi washiriki kuaga Miili ya Waliofariki katika Ajali iliyotokea Ngaramtoni Arusha

Image
  Na Innocent Natai Februari 27,2023 Katika Uwanja wa michezo wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Arusha, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru ,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPHPA Prof. Andrew Temu na wafanyakazi wa Mamlaka wameshiriki katika kuaga miili ya watu   kumi (10) kati ya ishirini na tano (25)waliofariki katika Ajali iliyotokea Jumamosi ya Februari 24, 2024 ikihusisha lori mali ya Kampuni ya KAY Construction ya Nairobi, Kenya na magari mengine madogo matatu, ilisababisha vifo vya watu 25 na kujeruhi wengine 21.

MCHECHU AIPONGEZA MAMLAKA YA AFYA YA MIMEA NA VIUATILIFU TANZANIA (TPHPA) KWA ONGEZEKO LA MADUHULI YA SERIKALI.

Image
Msajili Hazina Ndugu Nehemiah Mchechu, leo tarehe 20 Februari, 2024 ametembelea Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) iliyopo jijini Arusha, Tanzania. Katika  ziara hii, Bw. Mchechu alipokelewa na kufanya mazungumzo na Prof. Joseph Ndunguru ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo. Katika mazungumzo yao, Prof. Ndunguru amemueleza Msajili wa Hazina kuhusu mikakati ya mamlaka katika kuboresha utendaji na ukusanyaji wa maduhuli kwa niaba ya Serikali .  Bw. Mchechu amempongeza Prof. Ndunguru pamoja na menejimenti ya mamlaka hiyo kwa utendaji wenye tija na kimkakati  katika kusimamia viuatilifu ikiwa ni sehemu ya kusaidia wakulima na kuhakikisha uwepo wa usalama wa chakula nchini. Aidha, Msajili ameonesha kuridhishwa kwake na utendaji wa shirika kuendana na maelekezo aliyoyatoa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipokuwa akiongea na watendaji wakuu kwenye Kikao kilichofanyika Agosti, 2023. Rais Samia kupitia maono y...

MAFUNZO YA MATUMIZI SAHIHI NA SALAMA YA VIUATILIFU YAANZA RASMI IFAKARA

Image
  Febuari 12, 2024 Mratibu wa mafunzo Ndg. Jumanne Musalama amefungua mafunzo ya matumizi sahihi ya Viuatilifu yanayo tolewa na Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) kwa wafanya biashara na wakulima yenye lengo la kutoa elimu ya matumizi sahihi ya viuatilifu ili kuepuka madhara kwa binadamu na mazingira yanayotokana na matumizi yasiyo sahihi. Aidha akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Ndg. Jumanne alieleza faida na madhumuni ya mafunzo hayo hususani kwa wakulima na wafanya biashara   katika kutambua na kutumia viuatilifu kwa usahihi. Ambapo amesema yatasaidia wakulima na wafanya biashara kupata elimu juu ya njia sahihi za   matumizi bora ya Viuatilifu kwani matumizi bora ya viuawatilifu ni muhimu,pamoja na kupelekea mimea kuwa na afya na kuepuka athari mbalimbali Pia inasaidia kufungua masoko ya ndani na nje ya nchi kwa bidhaa zetu bora na kupelekea ongezeko la kipato kwa wakulima wenyewe na pia kwa taifa letu kwa ujumla kwani matumizi sahihi y...

Menejimenti ya TPHPA yatembelea vituo vya Ukaguzi Dar Es Salaam, Dkt. Osmund Ndomba aongoza

Image
 Na Innocent Natai TPHPA Febuari 10, 2024 Dkt. Osmund Ndomba kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru ameongoza wajumbe wa menejimenti ya Mamlaka hiyo kutembelea vituo ya ukaguzi vya TPHPA, Bandari ya Dar Es Salaam,Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar Es Salaam na Kituo cha Kitaifa cha Kudhibiti visumbufu kwa njia ya kibiolojia ziara hiyo ikilenga kuhimiza utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka na serikali kwa watumishi waliopo katika vituo hivyo Ziara hiyo imefanyika baada ya kuhitimishwa kwa Mafunzo ya Uongozi kwa wajumbe hao ya siku Moja yaliyoendeshwa na wakufunzi kutoka Taasisi ya UONGOZI