Tanzania yaanza kupiga hatua mpango wa Usimamizi wa Vifungashio vya Viuatilifu//Wadau wakutana kujadili mikakati

Arusha, Disemba 12, 2024 – Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph Ndunguru, amefungua kikao cha wadau kilichofanyika katika ukumbi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu jijini Arusha. Kikao hiki kililenga kutafuta suluhu bora ya usimamizi wa vifungashio vya viuatilifu, ili kuhakikisha afya ya binadamu na uhifadhi wa mazingira kwa sasa na katika siku zijazo. Katika hotuba yake, Prof. Ndunguru alisema kwamba kutokuwepo kwa usimamizi mzuri wa vifungashio vya viuatilifu kuna hatarisha mazingira na afya ya binadamu, hasa kwa wakulima wanapotumia viuatilifu bila ya kufuata taratibu bora za usimamizi wa vifungashio hivyo. Bwana Raphael Mwezi, Afisa Mwandamizi kutoka TPHPA, alifafanua kwamba kikao hicho kimejumuisha wadau kutoka sekta mbalimbali, akiwemo Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, wakulima, wataalamu kutoka TPHPA, na wadau wa viuatilifu. Lengo kuu la kikao hi...