TPHPA Yapokea Ugeni wa Wadau wa FVC, Wakiwemo Mabalozi na Maafisa Kutoka FAO Makao Makuu

Februari 26, 2025, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) ilipokea ugeni wa maafisa kumi na mmoja kutoka kwa wadau wa Michango ya Hiari ya Kifedha (FVC). Ujumbe huo ulijumuisha Mabalozi, Mwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa mjini Roma, Washauri Wakuu kutoka Mashirika ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa, pamoja na viongozi wa ngazi za juu kutoka Makao Makuu ya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), na uliongozwa na Mwakilishi wa FAO nchini Tanzania, Bi. Nyabenyi Tipo. Katika hotuba yake ya kupokea ugeni, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Dkt. Oshingi Shilla, alishukuru kwa ujio wa wadau hao na kueleza jinsi mamlaka na taifa lilivyojivunia misaada inayotokana na miradi mbalimbali inayotekelezwa na FAO Tanzania. Alitaja miradi kama vile Mradi wa Kuimarisha Huduma za Afya ya Mimea na Usalama wa Chakula, ambayo imesaidia kuboresha mifumo ya afya ya mimea na kuimarisha usalama wa chakula nchini Tanzania. "Ushirikiano huu umekuwa na manufaa makubw...