WATAALAM TPHPA WATAKIWA KUTUMIA KONGAMANO LA KIMATAIFA LA KONGWE MWITU(SANSEVIERIA) KUPATA TAALUMA NA MBINU ZA UTAFITI WA MMEA HUO

Na Mariam Makombe -TPHPA Hayo yamejiri katika kongamano la Kimataifa la SANSEVERIA linalofanyika katika ukumbi wa TPHPA ambapo Mgeni rasmi Dkt.Sospeter Kabululu akimuwakilisha Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka Prof.Joseph Ndunguru amewata wataalam wanaoshiriki kutumia fursa hiyo kujifunza Kwa umakini mbinu mbalimbali zinazotumika katika kutafiti mmea wa Kongwemwitu ambao una maajabu mengi na faida kubwa kwa binadamu na mustakabali wa dunia kwa ujumla. Akiongea mara baada ya kufungua Kongamano hilo amesema mkutano huu umekusanya Watafiti mbalimbali kutoka ujerumani,ufaransa,Uganda,Kenya, Zanzibar n.k ambapo kwa pamoja wanajadili kuhusu mmea huu wa Kongwemwitu ( Sansevieria) na kuona ni namna gani mikakati ifanyike katika kuhifadhi mmea huu wa kipekee ambao uko katika aina tofauti zaidi ya Mia moja usipotee katika uso wa dunia kutokana na shughuli za binadamu. "Mamlaka ya Afya ya mimea na Viuatilifu moja ya jukumu letu ni kuhifadhi mimea nasi tunabeba jukumu kuhakikisha mmea h...