Posts

Showing posts from November, 2024

Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA Apokea Makombe 6 yaliyopatikana Katika Mashindano ya Mei Mosi na SHIMMUTA 2024

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Profesa Joseph Ndunguru, amepokea jumla ya makombe 6 kutoka kwa Kamati ya Michezo ya Mamlaka hiyo, baada ya kufanya vyema katika mashindano mbalimbali yaliyofanyika kwenye mashindano ya SHIMMUTA jijini Tanga mwezi Novemba na sherehe za wafanyakazi (Meimosi 2024). Katika mashindano hayo, Mamlaka ya TPHPA ilifanikiwa kutwaa makombe katika michezo tofauti, ikiwa ni pamoja na: - Mchezo wa Bao: Mshindi wa Kwanza - Darts: Mshindi wa Pili - Karata: Mshindi wa Kwanza - Kukimbia kwenye Gunia: Mshindi wa Kwanza - Riadha: Mshindi wa Pili Akizungumza na Watumishi wa Mamlaka, Profesa Ndunguru alitoa pongezi kwa wachezaji wote walioshiriki na kushinda, akisisitiza umuhimu wa michezo katika kuboresha mahusiano kazini, afya njema, na kuongeza ufanisi wa kazi. Aliwataka watumishi wengine kujiunga na michezo ili waweze kufurahia faida zake, kama vile kujenga umoja na kukuza ustawi wa mwili na akili. Huu ni ushindi mkubwa kwa Mam...

Kanda ya Kaskazini yatolewa kimasomaso na TPHPA Mashindano ya SHIMMUTA 2024//Yatwaa Mataji Matatu huku ikiweka rekodi Maalumu

Image
Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imevunja rekodi kubwa katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Mashirika ya Umma, Taasisi, na Makampuni Binafsi (SHIMMUTA) 2024, yaliyofanyika mkoani Tanga. Mashindano haya ya 51 tangu kuanzishwa, yamejulikana kwa ushindani mkali, kujenga Afya za Watumishi na Ushirikiano miongoni mwao ukijumuisha ushiriki wa mashirika 95 na wanamichezo 4720 kutoka mashirika na Taasisi   Leo Novemba 24,2024 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo, alifunga mashindano hayo na kusisitiza umuhimu wa michezo katika kukuza afya na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi.  TPHPA inajivunia mafanikio na inashukuru wachezaji wake kwa kuleta heshima na mafanikio makubwa katika mashindano haya ambapo Bi. Rhoda Simon wa TPHPA alionyesha umahiri mkubwa katika mbio za magunia, akishinda kwa kasi ya kipekee na kumaliza mbio hizo kwa muda wa sekunde 28, na hivyo kutwaa taji la ubingwa ambapo leo amekabidh...

WAFANYABIASHARA WA VIUATILIFU MKOANI KATAVI WATAKIWA KURASIMISHA BIASHARA ZAO.

Image
Hayo yamejiri wakati wa kufunga mafunzo ya matumizi sahihi ya Viuatilifu kwa Wafanyabiashara na Wakulima Mkoani Katavi ambapo Mgeni rasmi Kaimu RAS wa Mkoa wa Katavi ndg.Florence Lungwa amewataka Wafanyabiashara wa viuatilifu kurasimisha biashara zao kwa kukata vibali na kufuata taratibu zote zinazotakiwa ikiwepo kupata mafunzo ili kuwa huru na biashara zao kwani kufuata taratbu kutawafanya wajiamini na kuwa huru katika kazi zao,lakini pia itakuwa wamefuata matakwa ya kisheria. Sambamba na hilo ndugu Florence  Lungwa amewataka kwenda kurekebisha makosa mbali mbali yaliokuwa yakifanyika au ambayo yangefanyika, "Mkarekebishe kulingana na taratibu mlizoelekezwa, msiruhusu watoto wadogo kuuza viuatilifu, msipimie watu viuatilifu, msichanganye viuatilifu na vitu vingine kama vyakula n.k, na mambo mengine yanayoathiri ufanisi wa viuatilifu na afya za watumiaji."alisema ndugu Florence Licha ya haho amewapongeza Washiriki waliofuzu vyema mafunzo hayo lakini pia TPHPA kwa ujumla kwa j...

Sekunde 28 zatosha kuifanya TPHPA kuwa bingwa Mchezo Wa Magunia Wanawake SHIMMUTA 2024

Image
Bi. Rhoda Simon aongoza mbio za Magunia Wanawake hivyo kuwa bingwa Katika Mbio za Magunia Wanawake katika Mashindano ya   Shirikisho la Michezo ya Mashirika ya Umma, Taasisi, na Makampuni Binafsi SHIMMUTA -TANGA Novemba 21, 2024  – Bi. Rhoda Simon ambaye ni Mfanyakazi wa Mamlaka (TPHPA) amekuwa bingwa kwakuwa mshindi wa kwanza katika mbio za magunia Wanawake zilizofanyika leo, katika mashindano ya  Shirikisho la Michezo ya Mashirika ya Umma, Taasisi, na Makampuni Binafsi . Ambapo alifanikiwa kumaliza mbio hizo kwa muda wa sekunde 28, na hivyo kutwaa taji la ubingwa wa  Mbio za magunia, ambazo zilijumuisha washiriki 36 kutoka taasisi na mashirika mbalimbali, zilifanyika kwenye uwanja wa michezo Sekondari ya Tanga Bi. Rhoda Simon alionyesha umahiri mkubwa, akiwaacha nyuma washindani wake kwa kutumia mbinu bora na kasi ya kipekee, na hivyo kushinda kwakuwa wakwanza katika mashindano haya yenye ushindani mkubwa. Mashindano ya mwaka huu yalishirikisha mashirika na ta...

UGUNDUZI VIUATILIFU HALALI KIZUNGUZUNGU KWA WAKULIMA,TPHPA YAWAPA MBINU KUEPUKA UBAMBIKWAJI

Image
TPHPA imeendelea kutoa elimu kwa Wakulima ,Wafanyabiashara wa Viuatilifu,Maafisa Ugani Mikoa mbalimbali ya Tanzania ambapo tarehe 18 mpaka 23 novemba  wapo Mkoani Katavi kutoa mafunzo ya matumizi sahihi na salama ya viuatilifu, pamoja na mada zingine Washiriki wamepewa mbinu sahihi za kugundua iwapo kiatilifu anachotaka kununua ni halali au feki. Akizungumza Mkufunzi kutoka TPHPA ndugu Ernaus Mwinuka amesema ni muhimu kila Mkulima kuhakikisha anakuwa na uelewa wa kutosha katika kugundua kiuatilifu ambacho ni halali na kisicho na mashaka ili kuepuka kuharibu mimea jambo ambalo linalopelekea hasara kubwa kutokana na uharibifu unaotokea baada ya kutumia kiuatilifu kisicho na sifa. Akiongelea mambo ya kuzingatia wakati wa ununuzi wa kiuatilifu  ndugu   Mwinuka amesema mnunuzi anatakiwa kuangalia taarifa za usajili kutoka Mamlaka ya Afya ya mimea na viuatilifu ,lakini pia aangalie taarifa za mwisho wa matumizi ya kiuatilifu husika,iwapo kiuatilifu kitakuwa hakina taarifa za us...

MCC Wahidi Kuimarisha Ushirikiano na TPHPA Kaimarisha Masoko ya Mazao Yetu Nje ya Nchi

Image
Wataalamu elekezi kutoka Millennium Challenge Corporation (MCC) leo walifanya ziara katika makao makuu ya Mamlaka ya Afya ya Mimea na  Viuatilifu  Tanzania (TPHPA), ambapo walifanya majadiliano na wataalamu wa mamlaka hiyo kwa lengo la kuelewa shughuli zinazofanyika na kuoanisha na programu ya MCC Threshold. Lengo kuu la majadiliano haya lilikuwa kubaini maeneo ya ushirikiano, hasa katika sekta ya uwezeshaji masoko (trade facilitation), ambapo walijadili mbinu za kuimarisha upatikanaji wa masoko ya mazao ya Tanzania nje ya nchi. Baada ya majadiliano, wageni walifanya ziara katika maeneo mbalimbali ya Mamlaka, ikiwemo Kituo cha Intelijensia ya Usalama wa Afya ya Mimea, Maabara ya Uchambuzi wa Masalia Viuatilifu na Maabara ya Kuhakiki Ubora wa Viuatilifu. Wataalamu hao kutoka MCC walishukuru kwa ushirikiano walioupata na kujibu maswali yote waliyokuwa nayo, na kuahidi kuendeleza mashirikiano baina ya pande hizi. Majadiliano hayo yamefanyika leo, tarehe 19 Novemba 2024, katika ma...

TPHPA yatwaa Ubingwa wa Bao Wanawake katika Fainali ya Mashindano ya SHIMMUTA - Tanga

Image
TANGA, Novemba 19, 2024 – Mchezo wa Bao katika Shirikisho la Michezo ya Mashirika ya Umma, Taasisi, na Makampuni Binafsi umeweza kutoa mchezaji mwingine aliyekamilisha safari yake ya mafanikio, ambapo Bi. Veneranda Edward, mfanyakazi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), amechukua ubingwa wa mchezo huo leo, baada ya kushinda fainali iliyofanyika kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Bi. Veneranda Edward alionyesha umahiri mkubwa katika mchezo wa Bao, akichuana na mchezaji kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) katika fainali iliyokuwa na ushindani mkubwa. Kwa mbinu nzuri na ustadi wa hali ya juu, Bi. Veneranda aliweza kumshinda mpinzani wake kwa pointi nyingi, akijinyakulia taji la bingwa katika mchezo huu wa Bao kwa Wanawake. Ushindi huu ni mwendelezo wa mafanikio ya wachezaji wa TPHPA katika mashindano haya, baada ya Bi. Rehema Abdala kutinga fainali ya Vishale (Darts) kwa wanawake, ambapo hata hivyo, Bi. Veneranda alijitokeza kama nyota wa siku, ak...